Katika kudumisha haki za binadamu na utawala wa sheria nchini Tanzania, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kimeendelea kufanya uangalizi wa utendaji kazi wa serikali ili kuhakikisha inatekeleza majukumu yake bila kukiuka misingi ya haki za binadamu na utawala wa sheria.
Mnamo Machi 7, 2018 Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kilipata taarifa za kushtusha za kutokuonekana kwa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) Ndugu Abdul Nondo na kufarijika baada ya kupata taarifa za kupatikana kwake mapema.
Hata hivyo taarifa za shutuma zilizoelekezwa kwa Abdul Nondo kutoka kwa jeshi la Polisi, Waziri wa Mambo ya Ndani pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam baada ya kujisalimisha kwa Jeshi la Polisi huko Iringa zimekishitua Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu na kuona ni vyema kufanya kumbushi ya kisheria kwa jeshi la polisi na viongozi hao kwa kukiuka sheria kama inavyofafanuliwa; Soma hapa
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.

LEAVE A REPLY
Your email address will not be published.